Posts

Featured post

KUNA GHARAMA YA KULIPA ILI UTEMBEE NA MUNGU

 KUNA GHARAMA YA KULIPA ILI UTEMBEE NA MUNGU 🔹Watu wengi sana wanapenda kutembea na Mungu katika maisha yao, na hicho ni kitu kizuri sana, lakini ni watu wachache sana ambao wanaelewa gharama wanayotakiwa kulipa ili wafanikiwe katika jambo hilo. 🔸Mungu anapenda kuona watu wake wanatembea pamoja nae kama walivyofanya wakina Henoko, Ibrahimu, Daudi n.k, lakini ana kanuni zake ambazo watu wake wanatakiwa kutembea nazo kila wakati. 🔹Kanuni kubwa ni kufanya mapenzi ya yake (yaani mapenzi ya Mungu) katika maisha yako. Yohana 8:28-29. 28. Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo.  29. Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.  🔹Unapotaka kufanya mapenzi ya Mungu na kutembea pamoja nae katika maisha yako, unatakiwa kufahamu na kuzingatia mambo yafuatayo; 1. LA...

MAARAFA NI NINI?

 Watu wengi wanasema unaangamia kwa kukosa maarifa lakini hawajui maana ya maarifa nini. Maarifa ni nini? Maarifa ni njia inayotumiwa kujitoa katika shida. Maarifa ni njia ya kupata kitu. Maarifa ni Elimu au ujuzi.  Biblia inazungumza hapo juu kwamba watu wengi wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, maarifa yanayozungumzwa hapa ni elimu na ujuzi sahihi wa Neno la MUNGU. Maana ya kwanza ya maarifa ni njia inayotumiwa kujitoa katika shida. Shetani ameleta shida nyingi sana na vifungo vingi sana kupitia mawakala zake wachawi, waganga na mizimu na watu wengi sana wameangamia kwa sababu tu wamekosa maarifa ya kuwatoa katika shida hizo. Biblia inajulisha ikisema kwamba Kumcha MUNGU ndio chanzo cha maarifa sahihi yanayoweza kumsaidia mtu ili atoke katika shida mbalimbali za kiroho, Hiyo iko Mithali 1:7 '' Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.'' Biblia inasema Ni wajinga peke yao ndio wanaoweza wakadharau Neno la MUNGU la kuwapa maarifa sahihi ...

Upendo wa MUNGU

 YESU NDIO NURU YA KWELI

KILA KONA IMEKUWA ((COVID-19

Image
DUH KILA KONA IMEKUWA ((Covid-19 Corona virus)) tambua Kabla ya corona kifo kilikuwepo na baada ya corona pia kifo kitakuwepo, Jitathimini ulipotoka, ulipo na unakokwenda.  2Wathesalonike 3:3 Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu. Utafanywa imara utalindwa na mwovu kwa shalti moja tu la kumpa YESU maisha yako nje ya YESU hakuna usalama aise!!!  Ndugu yangu mpendwa hivi ni kweli hivi ndivyo ulivyo? Ziko wapi nguo zako na viatu vyako vizuli? Iko Wapi gari yako V.X V.8🚗 uliyotamba nayo ukawamwagia watu maji Barabarani? Kwanini haupo kwenye nyumba yako nzuli ya thamani? Ngoja kwanza!! ziko wapi zile sherehe ulizokuwa ukizifanya na kusherekea kila kuchwapo? Iko wapi Digrii yako na Masters? Iko wapi passport yako na Visa? Mbona hauna hata ile ATM card 🏧 yako? Ooooh nini kimetokea kwenye meno yako na dimpozi zako? Iko wapi ile iPhone uliyoipenda Sana? Ziko wapi kumbukumbu zako za bank 🏦 (Bank statement)? Hivi nini kimetokea ...

AINA ZA HASIRA ZA WANAWAKE NA HEKIMA YA MKE KWA MUMEWE.

Image
AINA ZA HASIRA ZA WANAWAKE NA HEKIMA YA MKE KWA MUMEWE. 1. Kuna mwanamke ambaye akikasirika, huishia kulia tuu! 2. Lakini mwingine akichukia, anaongea saanaa muda wote hadi ikukere! 3. Mwanamke mwingine akikasirika, ananuna, haongei! Mtapishana tu kimya kimya. Mawasiliano kibubu-bubu. Shavu limejaa kama Kobra! 4. Mwingine akishikwa na hasira, period ya ghafla ghafla inafuata! 5. Wako wanawake ambao, akichukia, Atakachokishika usipokimbia anakutandika na anaweza kukuchoma na kisu,, majuto baadaye! 6. Mwanamke mwingine akikasirika, hasira zake zinaishia kwenye kuvunja-vunja vyombo. Au saa nyingine kugombeza- gombeza wafanyakazi na watoto! Dizaini hii, huwa ni wale waliokosa kukidhiwa haja za kihisia/ ndoa na waume zao! 7. Mwanamke mwingine akikasirika, Mtajuana kitandani panapo usiku, Nakwambia utaungama yoote! 8. Kuna wengine wakitibuliwa, hukimbilia kufunga mabegi na kuondoka! 9. Wapo ambao wakikasirika, wanagoma kupika! 10. Wengine wakichukia, wanaam...

KAMA GIDIONI

Image
1. Kama Gideon,  baadhi yetu tumefichwa na matatizo ambayo sisi ndio tunapaswa kuyatatua.  Tunazikimbia changamoto ambazo tuliumbwa ili tuzitatue. Toka Huko Mafichoni Aisee! 2. Wewe usipodhihirika, wengi wataathirika. Wito wa Mungu kwako ni muhimu sana, Hupaswi kuupuuzia. Viumbe vyote vinakusubiria udhihirike, tambua hilo, na Chukua hatua. 3. Weka woga kando, weka hofu kando, katika nchi yako ya ahadi lazima kuna majitu, lakini hayataweza kukudhuru. Wewe na Mungu ni jeshi kubwa, nenda kwa imani, nawe utaangusha milki za wafalme, na kuimiliki nchi yako ya ahadi. 4. Usikubali kukata tamaa. Usikubali kurudi nyuma. Usikubali kuvunjika moyo. Labda kwa wanadamu haiwezekani, lakini si kwa Mungu; ukiwa na Mungu, yote yanawezekana. 5. Wakati mwingine tunapitia mambo yanayotuumiza katika maisha, lakini mambo hayo hayo ndiyo yanaweza kuwa yanatuonesha kusudi na wito wa Mungu kwetu. Jiulize, mapito haya yatanifaa wapi? KUSUDI LAZIMA LITIMIE! Makubimsafiri@g...

UJUE UMUHIMU WA KUIOMBEA NAFSI YAKO

Image
UJUE UMUHIMU WA KUOMBEA NAFSI YAKO. Zaburi:42.2-6 Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako. Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu. Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu. Nafsi yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo nitakukumbuka, Toka nchi ya Yordani, na Mahermoni, na toka kilima cha Mizari. Bwana Yesu asifiwe sana sana. Biblia inatueleza kuwa Nafsi ni uhai; kwenye; Mwanzo:2.7 Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. Na ukisoma kwenye 42:2 utaona neno likisema hivi;  "Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU,Mungu a...